Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imefanikiwa kufanya upasuaji wa kwanza wa kifua kwa mgonjwa ili kuondoa uvimbe kwenye pafu kutumia tundu dogo moja uliowashirikisha watalaamu wazalendo ukiongozwa na Bingwa wa Upasuaji Kifua Duniani na mgunduzi wa upasuaji wa aina hiyo, Dkt. Diego Gonzalez Rivas kutoka nchini Hispania.